Watumishi Wanawake wa Tume ya Pamoja ya Fedha, waliadhimisha Siku ya Wanawake Duniani (ambayo huadhimishwa tarehe 8, Machi kila mwaka) kwa kutoa msaada wa mahitaji mbalimbali kwa Watoto wenye matatizo ya vichwa vikubwa na mgongo wazi wanaopatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MOI), siku ya tarehe 15 Machi, 2024.
Bi. Witness Mmbaga (kushoto) akimkabidhi Bi. Teofrida Mbilinyi (kulia) wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MOI) mahitaji yaliyotolewa na Watumishi Wanawake wa Tume ya Pamoja ya Fedha, walipotembelea wagonjwa siku ya tarehe 15 Machi, 2024.
Katibu wa Tume ya Pamoja ya Fedha, Bw. Ernest Maduhu Mchanga (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Watumishi wa Tume ya Pamoja ya Fedha baada ya Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi, uliofanyika tarehe 25, Agosti, 2023 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Tume, Jengo la Sukari, Dar es salaam. Wa kwanza kushoto (aliyekaa) ni Bi. Dorice A. Maembe - Katibu wa Baraza la Wafanyakazi, na kulia ni Bw. Francis R. Daggo – Katibu Msaidizi wa Baraza la Wafanyakazi.
Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la Tume ya Pamoja ya Fedha ambaye pia ni Katibu wa Tume akiongoza Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi, uliofanyika tarehe 25, Agosti, 2023 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Tume, Jengo la Sukari, Dar es salaam
Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la Tume ya Pamoja ya Fedha wakifuatilia kwa umakini Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi, uliofanyika tarehe 25, Agosti, 2023 kwenye ukumbi wa Mikutano wa Tume, Jengo la Sukari, Dar es salaam
Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la Tume ya Pamoja ya Fedha wakifuatilia kwa umakini Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi, uliofanyika tarehe 25, Agosti, 2023 kwenye ukumbi wa Mikutano wa Tume, Jengo la Sukari, Dar es salaam
Naibu Waziri Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Tume ya Pamoja ya Fedha, Kushoto ni Bi. Siima S. Kyarukuka - Mwandishi Mwendesha Ofisi na kulia ni Bw. George L. Maige - Afisa Utumishi, waliposhiriki Bonanza la Michezo ya Watumishi wa Umma (SHIMIWI) lililofanyika tarehe 12 Agosti, 2023 katika Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.
Maafisa Waandamizi kutoka wizara ya Fedha ya Marekani walipotembelea Tume ya Pamoja ya Fedha tarehe 17 Agosti, 2022.
Maafisa wa Tume ya Pamoja ya Fedha wakishiriki Maonesho ya Miaka 58 ya Muungano yaliyofanyika Zanzibar kuanzia Tarehe 22 Aprili, 2022 hadi Tarehe 06 Mei, 2022 katika viwanja vya Maisara.