Karibu tukuhudumie katika banda letu ambalo lipo katika maonesho ya Taasisi za Muungano, viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es salaam kuanzia tarehe 19 hadi 25 aprili, 2024.
Afisa wa Tume ya Pamoja ya Fedha Bw. George Lucas Maige, akitoa elimu kwa Mwananchi aliyetembelea banda la Tume katika maonesho ya Taasisi za Muungano ambayo yanafanyika viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es salaam kuanzia tarehe 19 hadi 25 aprili, 2024.
Karibu tukuhudumie katika banda letu la Tume ya Pamoja ya Fedha lililopo katika viwanja vya maonesho Nyamanzi – Zanzibar kuanzia tarehe 14 Aprili hadi 20 Aprili, 2024.
Mwanachi akipata elimu kutoka kwa Afisa wa Tume, Bi. Gugwa Juma Barisiba alipotembelea banda la Tume katika viwanja vya Nyamanzi – Zanzibar.
Rais wa Zanzibar, Mhe.Dkt. Hussein Ali Mwinyi, mkewe Mama Mariam Mwinyi na Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla wakimsikiliza Katibu Msaidizi wa Tume ya Pamoja ya Fedha Bw. Jonas Hungwi Nduttu (hayupo pichani), alipotembelea banda la Tume siku ya ufunguzi wa Maonesho ya Muungano katika viwanja vya Nyamanzi – Zanzibar.
Katibu wa Tume ya Pamoja ya Fedha Bw. Ernest Maduhu Mchanga (katikati) katika picha ya pamoja na Katibu Msaidizi Bw. Jonas Hungwi Nduttu (kulia), CPA. Rehema Ephron Mwakajube – Mhasibu Mkuu na Watumishi wa Tume ya Pamoja ya Fedha baada ya Ufunguzi wa maonesho ya miaka 60 ya Muungano katika viwanja vya Nyamanzi- Zanzibar.
Watumishi wa Tume ya Pamoja ya Fedha wakiwa tayari kupokea Wananchi wanaotembelea banda la Tume katika viwanja vya Nyamanzi – Zanzibar, siku ya ufunguzi wa Maonesho, tarehe 14 Aprili, 2024.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe. Mwanaasha Khamis Juma akisaini daftari la wageni, alipofanya ziara Tume ya Pamoja ya Fedha – Dar es salaam, aprili 15, 2024.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe. Mwanaasha Khamis Juma (watatu kutoka kushoto) katika picha ya pamoja na Katibu wa Tume Bw. Ernest Maduhu Mchanga (wapili kutoka kushoto), Kaimu Katibu Msaidizi Idara ya Huduma Saidizi Bi. Agness Joseph Bhwana (wa kwanza kushoto), na Katibu Msaidizi Idara ya Ufundi Bw. Jonas Nduttu (wa kwanza kulia), baada ya kuhitimisha ziara ya siku moja katika ofisi ya Tume – Dar es salaam.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe. Mwanaasha Khamis Juma (wanne kutoka kushoto) na Wajumbe wa Kamati ya Bajeti katika picha ya pamoja na Katibu wa Tume Bw. Ernest Maduhu Mchanga (watatu kutoka kushoto) na Menejimenti ya Tume ya Pamoja ya Fedha, baada ya kuhitimisha ziara ya siku moja katika ofisi ya Tume – Dar es salaam.