Menejimenti ya Tume ya Pamoja ya Fedha ikiongozwa na Katibu wa Tume, Bw. Ernest Mchanga, tarehe 28 Mei, 2026 imefanya ziara ya kukagua maendeleo ya ukarabati wa jengo la Ofisi za Tume unaoendelea katika eneo la Kivukoni, Dar es Salaam. Jengo hilo linatarajiwa kuwa makao mapya ya Tume ya Pamoja ya Fedha baada ya kuhama kutoka Ofisi zake za sasa zilizopo katika Jengo la Sukari, Posta, Dar es Salaam.
Menejimenti ya Tume ya Pamoja ya Fedha ikiongozwa na Katibu wa Tume, Bw. Ernest Mchanga, tarehe 28 Mei, 2026 imefanya ziara ya kukagua maendeleo ya ukarabati wa jengo la Ofisi za Tume unaoendelea katika eneo la Kivukoni, Dar es Salaam.
Jengo hilo linatarajiwa kuwa makao mapya ya Tume ya Pamoja ya Fedha baada ya kuhama kutoka Ofisi zake za sasa zilizopo katika Jengo la Sukari, Posta, Dar es Salaam.
Mhe. Shariff A. Shariff, Waziri wa Kazi na Uwekezaji wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (katikati) akipokea maelezo kuhusu majukumu ya Tume ya Pamoja ya Fedha kutoka kwa Bw. Haji K. Haji, Katibu Msaidizi Ofisi ya Tume Zanzibar, alipotembelea banda la Tume ya Pamoja ya Fedha siku ya ufunguzi wa Maonesho ya Miaka 62 ya Muungano, yanayofanyika katika Viwanja vya Mao Tse Tung, Zanzibar, kuanzia tarehe 21–27 Aprili 2026.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) akiwa katika kikao na Katibu wa Tume ya Pamoja ya Fedha, Bw. Ernest Mchanga (wa tatu kushoto), pamoja na Katibu Msaidizi, Idara ya Huduma za Kiufundi Bw. Jonas Nduttu (wa pili kushoto) walipomtembelea Mhe, Balozi Omar (Mb), ofisini kwake, Wizara ya Fedha, Treasury Square, Dodoma.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), (Katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Katibu wa Tume ya Pamoja ya Fedha, Bw. Ernest Mchanga (kulia), pamoja na Katibu Msaidizi, Idara ya Huduma za Kiufundi Bw. Jonas Nduttu baada na kufanya mazungumzo, walipomtembelea Mhe, Balozi Omar (Mb), ofisini kwake, Wizara ya Fedha, Treasury Square, Dodoma.