Katibu wa Tume ya Pamoja ya Fedha, Bw. Ernest M. Mchanga (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Tume walioshiriki hafla ya Usiku wa Mtanzania, iliyofanyika tarehe 26 Aprili 2026 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), Dar es Salaam.
Baadhi ya Watumishi wa Tume ya Pamoja ya Fedha katika picha ya pamoja kwenye Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani yaliyofanyika kwa ngazi ya Mkoa katika viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es salaam tarehe 01 Mei, 2026.
Katibu wa Tume ya Pamoja ya Fedha, Bw. Ernest M. Mchanga (katikati), akiwa na Katibu Msaidizi – Ofisi ya Tume Zanzibar, Bw. Haji K. Haji (kulia), pamoja na Katibu Msaidizi – Idara ya Huduma za Kiufundi, Bw. Jonas H. Nduttu (kushoto), wakiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Tume walipotembelea banda la Tume kwenye Maonesho ya Miaka 62 ya Muungano, yanayofanyika katika Viwanja vya Mao Tse Tung, Zanzibar, kuanzia tarehe 21–27 Aprili 2026.
Mhe. Dkt. Said H. Mrisho, Mkuu wa Wilaya ya Mjini akisaini daftari la wageni alipotembelea banda la Tume ya Pamoja ya Fedha katika Maonesho ya Miaka 62 ya Muungano, yanayofanyika katika Viwanja vya Mao Tse Tung, Zanzibar, kuanzia tarehe 21–27 Aprili 2026.
Mhe. Shariff A. Shariff, Waziri wa Kazi na Uwekezaji wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (katikati) akipokea maelezo kuhusu majukumu ya Tume ya Pamoja ya Fedha kutoka kwa Bw. Haji K. Haji, Katibu Msaidizi Ofisi ya Tume Zanzibar, alipotembelea banda la Tume ya Pamoja ya Fedha siku ya ufunguzi wa Maonesho ya Miaka 62 ya Muungano, yanayofanyika katika Viwanja vya Mao Tse Tung, Zanzibar, kuanzia tarehe 21–27 Aprili 2026.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) akiwa katika kikao na Katibu wa Tume ya Pamoja ya Fedha, Bw. Ernest Mchanga (wa tatu kushoto), pamoja na Katibu Msaidizi, Idara ya Huduma za Kiufundi Bw. Jonas Nduttu (wa pili kushoto) walipomtembelea Mhe, Balozi Omar (Mb), ofisini kwake, Wizara ya Fedha, Treasury Square, Dodoma.
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), (Katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Katibu wa Tume ya Pamoja ya Fedha, Bw. Ernest Mchanga (kulia), pamoja na Katibu Msaidizi, Idara ya Huduma za Kiufundi Bw. Jonas Nduttu baada na kufanya mazungumzo, walipomtembelea Mhe, Balozi Omar (Mb), ofisini kwake, Wizara ya Fedha, Treasury Square, Dodoma.