Mgeni rasmi katika kikao kazi Dkt. Ephraim O. Mdee (watatu kushoto) Katibu wa Tume Bw. Ernest M. Mchanga (watatu kulia) Katibu Msaidizi Bw. Jonas H. Nduttu (wa kwanza kulia) katika picha ya pamoja na Wataalam kutoka Wizara ya Fedha ya SJMT na Ofisi ya Rais Fedha na Mipango, Zanzibar baada ya kikao kazi kilichofanyika tarehe 19 Februari, 2026.
Wataalam kutoka Ofisi ya Rais Fedha na Mipango, Zanzibar Bi. Saida M. Omari – Afisa Mratibu wa Misaada (wa kwanza kushoto), Bw. Hamed N. Said - Mkuu wa Sehemu ya Usimamizi wa Deni la Serikali(wa pili kushoto), Bw. Salum S. Yahya – Mratibu Mkuu wa Misaada (wa tatu kushoto), wakifuatilia kikao kazi kilichojadili na kupokea maoni ya wadau kuhusu Ushirikiano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika Ukopaji na Usimamizi wa Madeni ya Serikali ya Nje ya Nchi, kilichofanyika tarehe 19 Februari, 2026.
Bw. Omary W. Khama - Kamishna Msaidizi, Idara ya Usimamizi wa Madeni kutoka Wizara ya Fedha ya SJMT (aliyeshika kipaza sauti) akitoa maoni katika kikao kazi kilichojadili na kupokea maoni ya wadau kuhusu Ushirikiano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika Ukopaji na Usimamizi wa Madeni ya Serikali ya Nje ya Nchi, kilichofanyika tarehe 19 Februari, 2026.
Katibu wa Tume ya Pamoja ya Fedha Bw. Ernest M. Mchanga akifuatilia kikao kazi kilichojadili na kupokea maoni ya wadau kuhusu Ushirikiano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika Ukopaji na Usimamizi wa Madeni ya Serikali ya Nje ya Nchi, kilichofanyika tarehe 19 Februari, 2026
Mgeni Rasmi Dkt. Ephraim O. Mdee, Mjumbe wa Sekretarieti ya Tume ya Pamoja ya Fedha kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania akifungua kikao kazi kilichojadili na kupokea maoni ya wadau kuhusu Ushirikiano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika Ukopaji na Usimamizi wa Madeni ya Serikali ya Nje ya Nchi, kilichofanyika tarehe 19 Februari, 2026.